Waziri Mkuu Abaini Semi Trela 44 Zikitaka Kutolewa Bandarini Bila Yakufuata Utaratibu....Amtaka IGP Sirro Awakamate Wahusika

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro kuwakamata, Bw. Bahman wa kampuni ya NAS na Wakala wa Kampuni ya Wallmark Bw. Samwel kwa kutaka kutoa bandarini magari makubwa aina ya semi tela 44 bila ya kulipa kodi kwa kutumia jina la Waziri Mkuu.

Pia Waziri Mkuu ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kutowasikiliza wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi kwa madai ya kupewa vibali vya msamaha wa kodi kutoka kwa viongozi wa juu Serikalini.

“Mtu asije hapa aseme amepewa kibali na Rais Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan au Waziri Mkuu cha kutaka kutoa mzigo wake bila ya kufuata taratibu. Akija mtu na taarifa hizo akamatwe mara moja na achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.”

Ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Novemba 29, 2017) alipofanya ziara ya ghafla bandarini baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara huyo aliyetaka kuutapeli uongozi wa TPA kutaka kutoa magari hayo yaliyoingizwa nchini mwaka 2015 kutoka nchini Uturuki.

Hatua hiyo imekuja baada ya Bw. Bahman wa kampuni ya NAS kutaka kupata msamaha wa  kodi kwa kuidanganya TPA kwa madai kwamba wamewasiliana na Waziri Mkuu na wasipotekeleza jambo hilo watapata matatizo.

Amesema Serikali inasisitiza watu kufuata sheria na taratibu za nchi ikiwa ni pamoja na kulipakodi  ipasavyo na inataka watendaji wake wafanye kazi bila ya kubugudhiwa, hivyo amewataka wafanyabiashara kufuata sharia za nchi na kwamba Serikali haina ugomvi nao.

Waziri Mkuu amefafanua kuwa mfanyabiashara huyo alitaka kuyatoa magari hayo bila ya kukamilisha malipo ya ununuzi kutoka kwenye kampuni Serin ya nchini Uturuki.

“Magari haya aliyalipia asilimia 30 tu kwa makubaliano ya kumaliza asilimia 70 iliyobaki baada ya kufika Tanzania na atakapokamilisha ndipo angepewa nyaraka ambayo inaonyesha jina la mwenye mzigo, aina ya mzigo na thamani  (bill of lading) inasaidia mteja kufanyiwa tathmini ya gharama za kulipia ushuru, lakin huyu bwana hajafanya hivyo”

Waziri Mkuu amesema kitendo cha kuyasajili magari hayo bila ya kuwa na nyaraka hizo ni kinyume cha sheria na pia kinaweza kusababisha kampuni iliyouza magari hayo ya Serin kutolipwa malipo yaliyobaki. 

Amesema jambo hilo halikubaliki kwa sababu linaweza kudhohofisha mahusiano mazuri iliyopo kati ya Tanzania na Uturuki kwani tayari kampuni hiyo imeshawasilisha malalamiko hayo katika ofisi za Ubalozi wa Uturuki nchini Tanzania.

“Uturuki wanawaamini sana wafanyabiashara wa Tanzania sasa huu ujanjaunja uliotumika katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuyasajili magari haya bila ya kuwa na bill of lading halisi unajenga sura mbaya kwa wafanyabiashara wengine waaminifu na watiifu wa sheria nawaagiza TRA kuchukua hatua kwa wahusika, hatuwezi kupoteza mahusiano na nchi kwa sababu ya utapeli wa mfanyabiashara mmoja.”

Pia Waziri Mkuu ametoa wito kwa Mawakala wa Forodha kuhakikisha wanakuwa makini katika kazi zao na Serikali haitawavumilia wababaishaji kwani inasisitiza wafanyabiashara kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo.

Awali, Mkurugenzi wa Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko alimueleza Waziri Mkuu kuwa pamoja na vitisho vya mfanyabiashara huyo kuwa wasipotekeleza matakwa yake watapata matatizo, lakini waliendelea kusimamia sheria na taratibu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMATANO, NOVEMBA 29, 2017
Share:

KAMANDA SIRO AJIGAMBA KUUPUNGUZA MTANDAO WA MAJANGILI WALIOKUWA WAKIUWA KIBITI,

MKUU wa jeshi la polisi nchini (IGP)Simon Sirro amewahakikishia wananchi mkoani Pwani kuwa silaha zote zilizochukuliwa na wahalifu wa ovyo ovyo huko Kibiti na Mkuranga zimerudi zote mkononi mwa dola na kusambaratisha mtandao wa kiuhalifu .
Aidha ametoa rai kwa wazazi na walimu kutoa taarifa kwenye vituo vya polisi mara watakapobaini kuna mwanafunzi mtoro ama hajaripoti shule kwa miezi kadhaa kwani wapo baadhi ya watoto wanaotumika kufundishwa uhalifu hata wakutumia silaha na watu wasiowema.
 
Pamoja na hayo IGP Sirro ,amesema vyombo vya ulinzi na usalama nchini vinashirikiana na nchi ya Msumbiji kupambana na wahalifu waliobainika kukimbilia nchini  humo wakitokea Tanzania.
 
Aliyasema hayo wilayani Kibaha ,mkoani Pwani ,katika ziara yake ya kikazi ya siku moja ambapo pia alizungumza na viongozi wa mashirika ya umma,wazee maarufu ,wastaafu mbalimbali na kamati ya ulinzi na usalama mkoani hapo.
 
IGP Sirro alieleza kuwa ,vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kupambana na yeyote atakaekuja kwa moto nae wataenda nae kwa moto na atakaekuja baridi wataenda nae baridi.
 
Alisema serikali imeshinda kwa hilo na hali kwa sasa ni shwari katika wilaya hizo.
 
IGP Sirro alieleza amepatiwa taarifa ya wanafunzi zaidi ya 1,300 mkoani hapo kuwa ni watoro na hawajulikani walipo hivyo wazazi washirikiane kusaidia jeshi la polisi kujua walipo.
 
“Kuna baadhi misikiti,makanisa yanadaiwa yanayotumia watoto hawa katika masuala ya kiuhalifu hivyo kuna kila sababu ya kuingia ndani kutafuta suluhu “
 
“Ni kazi yetu wazazi jamii na walimu kushirikiana ,na hapa ni muhimu wazazi wasaidie kusema watoto wao walipo ili kuwa na usalama” alisema .
 
Katika hatua nyingine IGP Sirro alielezea viongozi wa dini wana nafasi ya kuhakikisha wanatumia eneo lao kuhubiri amani .
 
“Tusidharau taarifa hata kama ni ndogo ,tusibweteke umoja ni nguvu tusaidiane kukomesha vitendo vya uvunjifu wa amani ” alifafanua IGP Sirro.
 
Akizungumzia changamoto ya wahamiaji haramu alisema wanashirikiana na uhamiaji kuusaka mtandao unaohusika kufanya biashara ya kusafirisha wahamiaji haramu .
 
IGP Sirro alisema hawatamvumilia yeyote anaekumbatia wahamiaji haramu kwani ni chanzo cha kusababisha kuleta magaidi  na kusafirisha bidhaa za haramu .
 
Alisema kwasasa wamejipanga kutaifisha mali za wafanyabiashara hao wa wahamiaji haramu na usafiri utaotumika kuwasafirisha.
 
Nae mkuu Wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,ameshukuru kuwepo Kwa kanda maalum kwani imeweza kuleta mafanikio makubwa .
 
Alisema kipindi cha nyuma kulikuwa na hali ya sintofahamu ,watu walisitiza shughuli zao za maendeleo ,biashara zilikwama,watu na baadhi ya viongozi walihama nyumba zao na wengine kulala saa 12 jioni kwa kuhofia mauaji.
 
Mhandisi Ndikilo alieleza sasa Kibiti na Rufiji hali ni shwarii kutokana na kuimarishwa ulinzi.
 
Aliwataka pia wawekezaji na wadau mbalimbali mkoani Pwani ,kujitokeza kushirikiana kusaidia kutatua changamoto zinazolikabili jeshi la polisi ikiwemo uhaba wa vitendea kazi ,usafiri na kujenga vituo vya polisi .
 
Mhandisi Ndikilo, alisema kuwa Mkoa huo umesheheni viwanda vya kutosha hivyo ni vyema kusaidia mambo hayo kwa manufaa ya wote wakati kukitokea uhalifu.
 
“Tukikumbwa na uhalifu tunapigia simu polisi, tusiwe Wa kwanza kulaumu wakati wa matatizo ,tukumbuke na kuwasaidia ili kufanikisha kazi zao kifanisi.;:” alisema mkuu huyo wa mkoa .
 
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Pwani ,(ACP)Jonathan Shanna alisema ziara hiyo ni neema kwao na wamepewa maagizo mbalimbali ambayo watayafanyia kazi.
 
Kamanda Shanna alisema wamemfikishia kero IGP zinazowagusa askari polisi ikiwemo upungufu wa makazi .

Advertisement
Share:

KENYATTA KUAPISHWA RASMI KUWA RAISI MPYA WA NCHI HIYO BAABA YA MVUTANO NA REILA ORDINGA.


Ni siku nyingine ambayo Taifa la Kenya leo linatekeleza shughuli muhimu ya kikatiba ya kumuapisha kiongozi wa taifa hilo kufuatia ushindi wake wa marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26 uliosusiwa na upinzani.

Uhuru Kenyatta leo anaapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa pili baada ya kuibuka mshindi kwenye uchaguzi mkuu.

Wageni mbalimbali wanatarajiwa kushuhudia sherehe za kuapishwa kwa kiongozi huyo wa Kenya huku ulinzi ukiimarishwa kila kona

Uchaguzi wa  uliofanyika Agosti ulifutwa  na mahakama kutokana na kile kilichotajwa kuwa uchaguzi usio huru na haki.

Marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26 ulimpatia Uhuru Kenyatta asilimia 98 ya kura huku waliojitokeza kushiriki katika shughuli hiyo wakiwa  na asilimia 39.

==>Tazama tukio hilo hapo chini


 
Share:

Makamu wa Rais Samia Suluhu amuwakilisha Rais Magufuli nchini Kenya Kushuhudia Kuapishwa kwa Rais kenyatta.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo asubuhi tarehe 28 Novemba, 2017 amewasili Mjini Nairobi nchini Kenya ambako anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba amepokelewa na Mhe. Balozi Robinson Njeru Githae wa Kenya na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Dkt. Pindi Chana.

Sherehe za kuapishwa kwa Mhe. Rais Uhuru Kenyatta zinafanyika katika uwanja wa Moi Kasarani Mjini Nairobi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Nairobi

28 Novemba, 2017
Share:

WAKATI IMEAKIA SIKU MOJA KURUDIA MNADA WA NYUMBA ZA LUGUMI, YONO AUCTION MART WATOA TAMKO,


Kampuni ya Udalali ya Yono imetangaza kuwa kesho, Novemba 24, 2017 itarudia upya mnada wa nyumba mbili za kifahari za mfanyabiashara Said Lugumi zilizoshindikana kuuzwa baada ya Dr. Louis Shika kuzinunua na kushindwa kuzilipia.

Nyumba zilizotajwa kurudiwa kuuzwa katika mnada ni Plot. No 47, iliyopo Mbweni JKT,  na nyingine iliyopo Upanga

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Yono Auction Mart, Scholastica Kevela ameeeleza kuwa kwa sasa kampuni ya Yono imeweka masharti magumu ili kuhakikisha kwamba hakuna atakayeibuka kuuharibu mnada huo.

“Niwakaribishe wateja ndani na nje ya nchi kuja kujinunulia nyumba zile kwa maana ujenzi ni mgumu..” amesema.

Aidha Bi Scholastica Kevela amewaonya wale wote wenye nia ya kuuharibu mnada huo kutofanya hivyo kwani hawatavumiliwa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Niseme kwamba mchezo ule tuliochezewa mara ya mwisho hautarudiwa tena. Kwa sasa hivi tumekuja na masharti magumu kwamba washiriki wote wawe aware na wanielewe,” amesema Bi. Kevela.

Masharti yaliyowekwa katika minada hiyo ni kwamba mshiriki atapaswa kujiandikisha kwenye kitabu maalum cha washiriki wa minada, baada yahapo atajaziwa ‘commitment form’ (fomu maalumu ya kushiriki mnada).

Baada ya hayo, vitambulisho vya mshiriki ikiwemo hati ya kusafiria (passport), leseni ya udereva na kitambulisho cha mpiga kura vitachukuliwa na kampuni.

Kila mshiriki halali atapaswa kulipa kiasi cha shilingi milioni 2 kupitia akaunti ya Yono ili kuthibitisha kuwa ana lengo la kushiriki. Kwa atakayeshinda mnada, fedha hizo (sh. 2 milioni) zitatumika kama sehemu ya malipo. Kwa ambao watakosa basi fedha zao zitarudishwa hapo hapo.

Kwa watakaoshiriki kuharibu mnada, hawatorudishiwa fedha hizo na watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kwa mshindi atakayepata nyumba atatakiwa kulipa hapohapo 25% ya gharama yote ya nyumba na 75% ya gharama inayobaki atapaswa kulipa ndani ya muda wa siku 14.

Yono Auction Mart wametoa onyo kubwa kwa watakaohusika kwa namna yoyote kuharibu minada hiyo kuwa watakamatwa na kufunguliwa kesi mahakamani kwa kuwa na nia ovu ya kukwamiha ukusanyaji wa kodi ya serikali
Share:

Waziri Mkuu Kassim majaaliwa Kufanya Ziara Ya Kikazi Mkoani Ruvuma .

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa (Mb) anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Ruvuma kuanzia tarehe 23 - 25 Novemba, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 22 Novemba 2017 na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema Mheshimiwa Waziri Mkuu atawasili mjini Songea siku ya Alhamisi tarehe 23 Novemba, 2017 na kupokelewa na viongozi wa Chama na Serikali katika Uwanja wa ndege Songea majira ya 7.00 mchana.

Baada ya kuwasili atapokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa na ile ya Chama Tawala Uwanja wa Ndege Songea. Kisha ataelekea Wilaya ya Namtumbo ambapo atafungua ghala la MIVARF, kuongea na Madiwani na watumishi wa Umma na baadaye ataongea na wananchi wa Namtumbo kwenye mkutano wa hadhara. 
Ijumaa tarehe 24 Novemba, 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu ataendelea na ziara yake kwa kuongea na wananchi wa kijiji cha Mchomoro kisha ataelekea Wilaya ya Tunduru ambapo atasalimia na wananchi wa vijiji vya Rahaleo,Milonde na Matemanga akiwa njiani kuelekea mjini Tunduru.

Aidha, Mheshimiwa Waziri Mkuu atatembelea kituo cha Afya cha Nakayaya, ghala la kuhifadhia Korosho na kupata taarifa ya Chama Kikuu Cha Ushirika TAMCU. Jioni Mheshimiwa Waziri Mkuu ataongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika mjini Tunduru katika uwanja wa michezo. Jumamosi tarehe 25 Novemba, 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu atahitimisha ziara yake mkoani Ruvuma na kurejea Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa Mndeme ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Ruvuma kujitokeza kwa wingi katika mapokezi kuanzia uwanja wa Ndege Songea atakapowasili Aidha amewaomba wananchi kujitokeza kwenye maeneo yote ambayo Waziri Mkuu atapita na kwenye mikutano ya hadhara ili wapate fursa nzuri ya kumsikiliza Mheshimiwa Waziri Mkuu na kupokea maelekezo atakayoyatoa.
Share:

TANZANIA YAIPIGIA MAGODI MAREKANI,YAAMUA KUZIFATILIA MALI ZAKE,IKIWA NI PAMOJA NA BOMBARDIA MOJA ILIYO SHIKILIWA.

Image result for bombardier
Tanzania imeiomba Mahakama ya Jimbo la Columbia kutupilia mbali ombi la Stirling Civil Engineering la kutaka kusajili hukumu mbili za Mahakama ya Kimataifa Usuluhishi ili kampuni hiyo ya Uingereza ikamate mali nyingine za Serikali zilizopo nchini Marekani.

Stirling, ambayo ni kampuni ya ujenzi iliyokatishwa zabuni ya kujenga Barabara ya Bagamoyo kutoka eneo la Wazo Hill kutokana na kutekeleza mradi huo chini ya kiwango, ilishinda ksi iliyofungua kupinga kitendo hicho msuluhishi akaagiza ilipwe dola 38 milioni za Kimarekani.

Kampuni hiyo ilisajili uamuzi huo wa msuluhishi nchini Uingereza na Uholanzi na kufanikiwa kushikilia ndege aina ya Bombardier Q400 iliyonunuliwa na Serikali na sasa inataka mahakama isajili hukumu mbili za mwaka 2015 na 2016 zisajiliwe Marekani ili ipate nguvu ya kushikilia mali nyingine.

Lakini Serikali ya Tanzania imeamua kupambana na kampuni hiyo mahakamani kuizuia isiendelee kukamata mali zake.

Kwa mujibu wa tovuti ya Law360, ambayo ni maalum kwa ajili ya habari za kisheria, Tanzania imewasilisha pingamizi, ikitaka mahakama hiyo isisajili hukumu hiyo ya Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi.

Katika hoja yake, Tanzania imesema mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kushughulikia ombi hilo la Stirling.

Serikali inasema ina kinga dhidi ya hukumu mbili zilizotolewa na mahakamani nchini Uingereza na Uholanzi ambazo kampuni hiyo inaomba zitambuliwe pia Marekani, ikisema kuwa ondoleo hilo la kinga linalotolewa na Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni, haiwezi kutumika.

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni inasema taifa la kigeni halitakuwa na kinga dhidi ya mamlaka ya mahakama ya Marekani katika mashauri yanayowasilishwa kwa ajili ya kuthibitisha tuzo za mahakama ya usuluhishi zinazoongozwa na makubaliano yaliyoidhinishwa na nchi yanayotambuliwa nchini Marekani.

Serikaloi inasema Stirling inataka kutambuliwa kwa hukumu za mahakama ya nje ili ziwe na nguvu, badala ya kuomba kutekelezwa kwa hukumu hizo.

“Kuna tofauti inayotambulika vizuri kati ya kuthibitisha tuzo ya msuluhishi, kwa upande mmoja, na kutambua hukumu ya mahakama ya nje, kwa upande mwingine,” tovuti hiyo inakariri hoja hizo za Serikali.

“ingawa tuzo ya msuluhishi na hukumu ya mahakama zinalingana kwa kiasi kikubwa, hata hivyo zina tofautiana.”

Kwa hiyo, Serikali inasema Stirling haiwezi kutumia mwanya huo, kuomba utekelezaji wa hukumu hizo.

Kampuni hiyo inadai kuwa kitendo cha Serikali ya Tanzania kukubali kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi, kiliondoa kinga hiyo na kuipa yenyewe haki ya kulipwa fidia hiyo.

Mwaka 1999 Serikali iliipa kandarasi kampuni ya Impresa Ing. Fortunato Federici SpA (IFF) ambayo baadaye ilinunuliwa na Stirling, kukarabati barabara ya Wazo Hill-Bagamoyo, lakini baadaye ikatimuliwa.

Mwaka 2004 kampuni hiyo ilifungua kesi Mahakama ya Usuluhishi wa Kimataifa na hukumu ilitolewa mwaka 2009 na 2010, lakini Serikali haikulipa fidia iliyopendekezwa na kuilazimu kukazia hukumu Uingereza na Uholanzi.

Novemba 2015, mahakama nchini Uingereza iliridhia utekelezaji wa hukumu hiyo na Uholanzi ilifanya hivyo Desemba 2016
Share:

Kutoka singida>> Mhasibu feki atiwa mbaroni kwa wizi wa Tsh. 873,000

Na Nathaniel Limu, Singida
 Mhasibu wa hospitali ya mkoa mjini Singida aliyeachishwa kazi kwa kosa la kumiliki vyeti feki, Edith Talasi (49) mkazi wa Minga,anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kuvunja milango ya ofisi yake ya zamani na kuiba shilingi 873,000 taslimu, kwa kutumia funguo bandia.

Talasi  ambaye imelelezwa kwamba alifanya kazi hospitalini hapo kwa  muda na baadaye alirejeshwa kwenye kituo chake cha kazi manispaa ya Singida,kwenye wizi huo, alimshirikisha mlinzi wake wa nyumba ya kulala wageni Nandau, Antony Felix (51).Mlinzi huyo naye anashikiliwa na polisi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, ACP Debora Magiligimba, alisema tukio hilo limetendeka Novemba, 21 saa 6.30 usiku huko katika hospitali ya mkoa mjini hapa.

Alisema siku ya tukio muuguzi wa zamu Shamir Omari (27) akitokea maeneo ya mapokezi akielekea wodini, alimwona mtu akiwa amesimama karibu na ofisi ya mhasibu, alisimama akamsalimia na mtu huyo aliondoka.

“Muuguzi huyo aliamini kuwa mtu aliyemwona,huenda alikuwa  mgonjwa au mtu aliyeleta mgonjwa hospitalini.Lakini aliporudi,alimwona mtu yule yule amerudi eneo lile lile, kitendo kilichopelekea amshuku kuwa sio mtu mzuri,” alisema kamanda huyo.

Alisema muuguzi huyo baada ya kumtilia shaka mtu huyo, alitoa taarifa kwa mlinzi wa zamu wa hospitali hiyo, Abubakari Jumanne,ambaye alimweka chini ya ulinzi mtu huyo.

ACP Magiligimba alisema hata hivyo mtu huyo alijitetea kuwa amefika hospitalini hapo, kwa ajili kuchoma sindano na kuonyesha dawa ya unga na kichanganyio chake.

“Wakati wanaendelea na mahojiano hayo,waliona makufuli  mawili ya mlango wa nje/grili yapo chini na mlango huo wa chuma upo wazi. Mtuhumiwa mlinzi Antony alieleza kuwa bosi wake (mtuhumiwa Edith) kwa wakati huo,alikuwa ndani ya ofisi ya mhasibu amejifungia ndani,” alisema.

 Akifafanua  alisema  jeshi la polisi baada ya kupata taarifa ya wizi huo, liliweza kufika eneo la tukio na kukuta mlango wa ndani ukiwa umefungwa kwa ndani.

“Walipoamuru mhasibu afungue mlango huo kwa kutumia funguo zake,walimkuta mtuhumiwa (Edith) akiwa amejibanza kwenye kona ya mlango na watumishi wa hospitali hiyo, waliweza kumtambua. Alipohojiwa ameingiaje humo ndani,alionyesha funguo saba (07) na zilipojaribiwa ziliweza kufungua milango yote ya ofisi ya mhasibu,” alisema Magiligimba.

Alisema pamoja na wizi huo wa shilingi 873,000,imeelezwa kwamba aprili mwaka huu,wahasibu wa hospitali hiyo,walibaini upotevu wa shilingi 1,800,000.Oktoba mwaka huu,pia walibaini upotevu wa shilingi 3,600,000.

Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. David Mwasita,amekiri kutokea upotevu huo lakini wahasibu katika wakati huo,waliweza kuziba upotevu huo, kwa fedha zao za mishahara.

Ameeleza kuwa wahasibu hao walilazimika kutoa fedha zao binafsi, na wasingeweza kutoa taarifa ya upotevu huo, kwa vile milango na kasiki, ilikuwa imefungwa kama kawaida.

ACP Magiligimba amesema kwa sasa wanaendelea kuwahoji watuhumiwa hao na baada ya kumalizika kwa mahojiano hayo,watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili
Share:

Ni vita ya maneno sasa>>GodBless Lema Amtaka Kafulila Amshauri Mkewe Naye Ajiondoe CHADEMA

Image result for lema na kafulila
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia CHADEMA Godbless Lema, amefunguka kuhusu kitendo cha David Kafulila kuhama CHADEMA na kusema ana amini atamshauri mke wake naye afuate nyayo zake.

Kwenye ukurasa wake wa twiter Godbless Lema ameandika ujumbe akisema Kafulila ni rafiki yake wa karibu, lakini kwa namna alivyoamua hana shaka atamshauri mke wake ambaye ni mbunge kupitia chama cha CHADEMA, kufanya kama yale aliyoyafanya.

"David Kafulila ni rafiki yangu, nafikiri kwa namna hii alivyoamua ataweza bila shaka kumshauri Mbunge wa Chadema, Jesca Kishoa (mke wake) kufikiri kama yeye, hii inaweza kusaidia maoni yake juu ya uamuzi aliouchukua leo na kuthibitisha ukweli huu kama hupo", ameandika Godbless Lema.

Jana David Kafulila ametangaza kukihama chama cha CHADEMA akidai vyama vya upinzani havina nia ya kupambana dhidi ya ufisadi, lakini mke wake Jesca Kishoa ambaye ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA bado hajazungumza chochote.

t
Share:

RC Makonda Atembelea Ofisi Za Clouds Media Group na kuongea na uwongozi na kutoa pole kwa kusaga

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dar es Salaam mapema leo ametembelea Ofisi za Clouds Media Group kutoa pole ikiwa ni siku moja baada ya ofisi hizo kukumbwa na janga la moto uliotokea hapo jana majira ya saa nne asubuhi.

Viongozi wengine wa serikali waliofika ofisini hapo ni Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni, Ally Hapi na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta.

Hata hivyo, tayari matangazo ya vituo vya Clouds FM na Clouds TV yamerejea hewani baada ya kupotea siku nzima  jana kutokana na hitilafu iliyosababishwa na moto huo ambao chanzo chake hadi sasa hakijajulikana.

Advertisement

Share:

Rais Magufuli Akutana Na Rais Wa Zanzibar Dkt. Shein Ikulu Jijini Dar Es Salaam Leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana na kufanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 22, 2017-PICHA NA IKULU

Advertisement
Share:

KAFULILA AIHAMA CHADEMA NA KUANGUKIA MIKONONI MWA MAGUFULI,

Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 David Kafulila amejivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taarifa ya Kafulila kuondoka CHADEMA imetolewa leo kwa vyombo vya habari, na kueleza kwamba hana imani tena na vyama vya upinzani katika kupambana na ufisadi.

David Kafulila anafahamika zaidi kwa kuibua mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa kwa kuibua bungeni suala la Escrow.
Share:

Zoezi la Kusafisha na Kuunga Bomba la Gesi-KINYEREZI 1 NDIO CHANZO CHA UMEME KUKATA KATA OVYO.


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), linawataarifu Wateja wake kuwa  Jumamosi Novemba 18 na leo Jumapili Novemba 19, 2017 kuna usafishaji na kuunga bomba kubwa la Gesi katika Mitambo ya Kinyerezi I, sambamba na zoezi hilo pia yanafanyika maandalizi ya kukiunganisha Kituo cha Kinyerezi II, kuanzia Saa:02.00 Asubuhi hadi saa 11.00 Jioni, kama tulivyowatangazia.

Kutokana na kazi hiyo kutakuwa na upungufu wa umeme katika Gridi ya Taifa, hivyo baadhi ya Wateja waliounganishwa katika Gridi ya Taifa wa maeneo mbalimbali Nchini watakosa huduma ya umeme.

Zoezi hilo linaendelea kwa ufanisi mkubwa na uharaka ili kurejesha huduma ya umeme kwa wakati.

TAHADHARI
Kutokana na kazi hii Wananchi mnaombwa msipite karibu na eneo la Mitambo ya Kinyerezi, kutokuwasha moto, kutokufanya shughuli za uchomeleaji vyuma pamoja na shughuli nyingine yoyote yenye viashiria vya moto, ili kujikinga na madhara yanayoweza kutokea iwapo shughuli tajwa zinafanyika maeneo yaliyo karibu na Mitambo.

Shirika limesha fanya taratibu zote za ki usalama katika eneo la Mitambo.
Share:

MUGABE NDIO BASI TENA,WANANCHI WAUNGANA NA JESHI KUMTAKA MUGABE KUIACHIA NCHI HARAKA.

Maelfu ya raia wa Zimbabwe jana walijitokeza barabarani hasa mjini Harare wakijiandaa kwa mkutano mkubwa unaoungwa mkono na chama tawala ZANU-PF katika jitihada za kuongeza shinikizo la kumtaka rais Mugabe ajiuzuulu,wakishikilia mabango yaliyoandikwa Mugabe Must Go.

Zanu-PF ndio chama kilichomsaidia Mugabe kuwa madarakani nchini kwa takriban miaka 40.

Lakini sasa inabidi wamshinikize ajiuzulu kufuatia mpasuko mkubwa katika chama tawala.

Kikubwa kinachozozaniwa ni nani atakayemrithi rais Mugabe atakapoochia madaraka.

Jeshi la nchi hiyo lilichukua hatamu za kiserikali na kumweka Mugabe chini ya kizuizi cha nyumbani tangu juzi na wamekuwa wakifanya mazungumzo ya kina.

Mugabe angependelea mkewe kumrithi lakini wapiganiaji wa uhuru nchini humo wanamtaka aliyekuwa makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambaye Mugabe alimfuta kazi wiki iliyopita, kutokana na uhasama mkubwa baina yake na mkewe rais Mugabe uliotokana na upiganiaji huo wa madaraka.

Zaidi ya hayo Bw. Mugabe angependa kuendelea kuwa uongozini hadi chama kitakapofanya mkutano wao mkuu mwezi ujao. 
Share:

KIMENUKA,>>POLISI WATUMIA VIFARU NA BUNDUKI BARIDI KUTAWANYA WAFUASI WA LOWASSA MKOANI KILIMANJARO.


Polisi Mkoa wa Kilimanjaro wamelazimika kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi kumwezesha mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kupata nafasi ya kupita mjini Moshi.
 
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walitumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi waliokuwa wamefunga barabara.
 
Takriban mabomu manne ya kutoa machozi yalifyatuliwa saa 10:30 jana jioni ya  Jumamosi Novemba 18,2017  katika eneo la Soko la Manyema ambako Lowassa na msafara wake alikuwa apokewe ili kuelekea kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za udiwani eneo la Pasua Relini.
 
Kabla ya Lowassa kufika, vijana madereva wa bodaboda walipita katika Barabara ya J.K. Nyerere.
 
Vijana hao walipopita mzunguko wa magari wa Coca Cola saa 10:15 jioni, gari la polisi aina ya Toyota Land Cruicer likiwa na polisi wenye mabomu ya machozi lilionekana likiwafuata.
 
Haikupita dakika 15, ndipo kulisikika milio ya mabomu katika eneo la Manyema ambalo ni njia panda ya kuelekea eneo la mkutano.
 
Katibu wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema ambaye yuko katika msafara wa Lowassa, alisema eneo la Manyema lilikuwa halipitiki kutokana umati wa watu.
 
Lema alisema ni kutokana na hali hiyo, ili kumwezesha Lowassa na msafara wake kupita, FFU walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah alisema mabomu hayo yamepigwa ili kupunguza idadi ya watu waliokuwa wamefurika kwenye eneo hilo na kumuwezesha Lowassa kupita.
 
“Alikuwa hana njia ya kupita, watu walifurika kiasi kwamba hata Lowassa mwenyewe asingeweza kupita, tulifanya hivyo kuwapunguza na ameshapita ameenda zake kwenye mkutano,” alisema
Share:

USIOGOPE KUDHARAULIKA,WALA KUCHEKWA,MAFANIKIO HUJA KWA MAJARIBU MENGI,HATIMAE DR SHIKA,TAJIRI MTATA, AWA BAROZI MPYA WA SOKABETTI.


Fungua hiyo link ya brue utamuona dr shika akiwa uwanja wa taifa akifanya mambo yake,.utacheka.
https://youtu.be/tGYxBmoaGZE
Share:

HAYAWI HAYAWI,SASA YAMEKUWA,YULE TAJIRI MTATA,DR SHIKA,SASA KUZILIPIA ASILIMIA 25 NYUMBA ZA LUGUMI

Bilionea wa nyumba za Lugumi aliyeteka vichwa vya habari siku za hivi karibuni, Dk. Louis Shika, amekamilisha malipo ya bima kwa ajili ya kutumiwa fedha zake kutoka nchini Urusi..

Dk. Shika aliingia matatani baada ya kushinda mnada wa uuzwaji wa nyumba za Said Lugumi hali iliyosababisha kukamatwa na polisi, lakini binafsi alisisitiza kuwa fedha hizo anazo na sasa anaelekea kuthibitisha hilo kwa kufanya mchakato wa kutumiwa fedha.

Waandishi wa habari walimkuta Dk. Shika akiwa katika huduma za mtandao wa internet katika shirika la Posta Jijini Dar es Salaam, ambao walikuwa katika ziara ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye na kujikuta hata mwenyewe akimshangaa bilionea huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kutuma taarifa za miamala hiyo, Dk. Shika amesema ametuma kiasi cha dola 100 ambapo anatarajia muda si mrefu ataweza kutumiwa fedha zake na kwenda kulipia asilimia 25 ya fedha zinazotakiwa katika nyumba hizo.
Alipoulizwa kama fedha hizo zikichelewa na kukuta mchakato huo wa malipo umepita, amesema kwa kujiamini, atanunua nyingine kwani Dar es Salaam kuna nyumba nyingi zinazouzwa siyo lazima hizo za Lugumi.

Kiasi hicho cha fedha, amekilipa kwa kwa Benki ya Equity kwenda Benki ya Bankok nchini Thailand, mchakato utakaomwezesha kutumiwa fedha zake na kuweza kununua nyumba hizo.

Katika hatua nyingine Dk. Shika alisifia huduma za shirika hilo na kueleza kwamba ndiyo hutuma huduma za internet katika kutuma nyaraka zake mbalimbali ndani na nje ya nchi
Share:

BOT>>HII NDIO SABABU YA BENK YA AMANA KUFUNGWA.

Share:

BURUNDI IPO TAYARI KUWAREJESHA WAKIMBIZI WALIOKIMBILIA TANZANIA NYUMBANI.

Serikali ya Jamhuri ya Burundi imesema ipo tayari kutoa ushirikiano wa hali na mali katika kuhakikisha zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi waliopo nchini Tanzania wanarejea nchini Burundi kwa haraka ili wakaijenge nchi yao.

Haya yamezungumza na Waziri wa mambo ya Ndani na Mafunzo ya Uzalendo kutoka Jamhuri ya Burundi Mhe. Pascal Barandagiye, alipozuru katika kambi za Nyarugusu, Nduta na Mtendeli kutoa ujumbe wa kuwaasa kurejea wakimbizi nchini kwao Burundi.

Tangu zoezi la urejeaji wa wakimbizi lilipoanza mwezi septemba 2017 kwa awamu ya kwanza jumla ya wakimbizi 8347 wameshasaidiwa kurejea nchini kwao Burundi sawa na asilimia 100.3 ya lengo ya urejeshwaji kwa awamu ya kwanza.

Aidha, mwanzoni mwa mwezi Novemba wakimbizi wapatao 33,948 walijiandikisha kurejea nchini kwao Burundi lakini kutokana na kasi ndogo na taratibu ndefu zinazofanywa na Shirika la kuhudumia wakimbizi Duniani UNHCR wakimbizi waliojiandikisha wameanza kusitisha nia yao ya kurejea kwani hawaoni jitihada zinazofanywa kuwarudisha, ambapo jumla ya wakimbizi 735 kati ya 33948 wamesitisha nia yao ya kureja kwa hiari.

Hali hii inatajwa na viongozi wa Burundi kuwa inachelewesha zoezi kwani wakimbizi wanaorejeshwa kwa mujibu wa mpango wa urejeaji ni ndogo. Mhe. Pascal Barandagiye amesema serikali ya yake ipo tayari kutoa magari kwaajili ya kuwasafirishwa wakimbizi kurudi nchi mwao, pamoja na kuwapa huduma muhimu za kibinadamu.

 “zoezi la urejeshaji wa Wakimbizi kwa hiari linaenda polepole mno tofauti na matarajio, shirika la kuhudumia wakimbizi duniani UNHCR linaenda kwa kasi ndogo tofauti na ilivyotarajiwa, hivyo kutokana na zoezi hilonkuenda taratibu Serikali ya Burundi ipo tayari kutoa magari, fedha na huduma nyingine za kibinadamu ili kusaidia kuweza kuharakisha zoezi la kurejesha wakimbizi waliojiandikisha kurejea kwa hiari nchini Burundi” alisisitiza Barandagiye.

Akiongea katika nyakati tofauti tofuti katika kambi za nyarugusu, nduta na mtendeli, amewahakikishia wananchi wa  kuwa Amani nchini mwao ipo ya kutosha hakuna vurugu na serikali ya Burundi inawahitaji ili warejee kuenga taifa lao hakuna haja ya kuendelea kubaki makambini.

Wakimbizi wakiongea kwa nyakati tofauti wamemhakikishia kuwa bado wanapenda nchi yao Burundi, na wanatamani kurejea Burundi, lakini changamoto inayowakabili hadi kukata tamaa ya kurudi ni taratibu ndefu zinazowachelewesha kurejeshwa mara tu baada ya kujiandikisha
 Akiongea kwa niaba ya Wakimbizi walioko kambi ya Nduta Bw. Suleima Hamisi (65) ambaye amekuwa Mkimbizi mara Sita kwa nyakati tofauti tangu mwaka 1972 alisema “ Sisi tulishajiandikisha Zaidi ya miezi mine sasa ili tuweze kurejeshwa cha kushangaza hadi sasa badotupo makambi”  ameiomba serikali ya Burundi na Tanzania na Shirika la kuhudumia wakimbizi wakae na kuzungumza kwa pamoja juu ya mustakabali wa kuwarejesha haraka wenye nia ya kurudi Burundi.

Akitoa taarifa kwa Waziri wa mambo ya ndani na mafunzo ya uzalendo wa Burundi na Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Jamuhuri ya Muungani wa Tanzania, Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu ikiyopo Wilayani Kasulu alisema kumekuwa na mwitikio Mkubwa wa wakimbizi wanao jiandikisha kurejea kwa hiari nchini Burundi lakini changamoto imekuwa taratibu ndefu zinazochelewesha kurejea kwao zinawafanya baadhi yao kuahirisha kurejea kutokana na kusubiri kwa muda murefu.

Serikali ya Burundi pia imedai Shirika la kuhudumia wakimbizi Dunia UNHCR linatakiwa kubadilisha utaratibu wa kuwapatia au kuwagawia vyakula na pesa wakimbizi wanapokuwa wanarejea wameomba zoezi hilo lifanyike wakati tayari wakimbizi wakishapatiwa nyumba na maeneo yao ya makazi kuepusha kukaa kwa muda mrefu kwenye vituo vya kuwapokelea.

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema serikali ya Tanzania itahakikisha wakimbizi waliopo nchi wanahifadhiwa kwa mujibu wa makubaliano ya taratibu za kimataifa na wale wanaopenda kurejea kwa hiari itashirikiana na UNHCR,  nchi ya Burundi ili kufanikisha zoezi hilo. Hatua ya kuwarejesha wakimbizi katika nchi yao ya asili ni moja kati ya suluhisho la kudumu la ukimbizi kwa mujibu wa sharia ya kimataifa ya wakimbizi ya mwaka 1951 na Sheria ya Wakimbizi ya Tanzania yam waka 1998 kifungu Na. 3

Zoezi la kurejea kwa wakimbizi nchini mwao waliopo Tanzania lilianza kuratibiwa mara tu baada ya tamko la viongozi rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunzinza walipo kutana Mwezi Julai 20, 2017 na kutamka kuwa wakimbizi waliopo Katika Makambi nchi Tanzania warejee nchini kwao kwani Burundi kuna amani ya kutosha.

Hadi sasa idadi ya wakimbizi walioko katika Mkoa wa Kigoma ni 210,005 na waomba hifadhi 26,410, kati ya hao 95,243 wapo kambi ya Nduta, 48147 kambi ya Mtendeli na 66615 Nyarugusu, aidha waombahifadhi wote wapo katika kambi ya nduta.
Share:

LIKE FB PAGE

bonyeza hapa

Total Pageviews

Blog Archive

Pages